TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa, Uchaguzi Mkuu utafanyika
kama ulivyopangwa na haiwezi kusegeza mbele tarehe ya uchaguzi huo
kutokana na suala hilo kuwa ni la kikatiba.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji
Mstaafu Damian Lubuva akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar
es Salaam, kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Manunuzi na Logistic, Gregory
Kaijage na kushoto ni Naibu Katibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na
Mkuu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), Sisti Chriati.
Akizungumza na
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Tume ya
Taifa ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema
kuwa wanasiasa wamekuwa na kauli ambazo zinawafanya wananchi wapate hofu
wakati suala hilo kuhairisha uchaguzi halipo katika tume.
Baadhi ya Wandishi wa habari waliohudhuria katika mkutano wa habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi jijini Dar es Salaam.
jaji
Lubuva ameongeza kuwa wanasiasa wanatakiwa kuangalia maneno ambayo
wanayatoa kwani hayana msingi, wanatakiwa watoe sera zao za vyama kwa
wananchi na sio kuisemea tume mambo ambayo hayana ukweli wowote.
Kumekuwa na shauku ya wananchi kwa sisi kushirikiana na vyama vingine
vya siasa ili kufanikisha malengo yetu ya kuleta mapinduzi ya kiuchumi
kwa kuubomoa mfumo wa uchumi unaonyonya wananchi. Msimamo wetu upo
wazi na tumeueleza mara kadhaa.
1 tunaunga mkono juhudi zozote za kushirikiana kwa vyama na hili
linathibitishwa na jina letu ALLIANCE na Msimamo wetu kuhusu mabadiliko
ya Katiba.
2 tunataka ushirikiano utakaonufaisha wananchi na sio ushirikiano wa kugawana nafasi za uongozi.
3 hatuna shida na Tupo tayari kushirikiana na chama chochote kilicho
tayari kushirikiana na sisi ikiwemo UKAWA ili kuunganisha nguvu kuitoa
CCM kwa malengo ya kujenga uchumi shirikishi wenye kuzalisha ajira
nyingi na bora, wenye mfumo wa hifadhi ya jamii kwa wananchi wote na
wenye kutokomeza umasikini.
Kiongozi wa chama cha upinzani
nchini Afrika Kusini cha Democratic Alliance,DA, amesema hatagombea
katika uchaguzi wa chama hicho mwezi ujao.
Helen Zille kiongozi wa chama cha Democratic Alliance cha nchini Afrika Kusini
Helen Zille amesema ni wakati muafaka kwake kutogombea, akisema kuwa DA watanufaika na mchango wa vijana. Atabaki kuwa waziri mkuu wa jimbo la Western Cape hadi mwaka 2019.
Bi Zille, mwandishi wa habari wa zamani na mwanaharakati wa kupinga ubaguzi wa rangi amekiongoza chama hicho tangu mwaka 2007.
Wanavyuo
hao wapatao 1500 walioungana toka vyuo vikuu na vyuo vya kijamii Iringa
wamesema kuwa wanamuomba Lowasa agombee uraisi na wako tayari kumuunga
mkono. Wameyasema hayo wakiongea na waandishi wa habari wakati
wakijitolea damu na kufanya usafi ktk hospitali ya rufaa ya mkoa wa
Iringa.
Picha Kiongozi wa ACT Wazalendo Ndugu Zitto Z.Kabwe akihutubia umati
mkubwa wa wana Songea waliohudhuria kumsikiliza,ikiwa ni ziara yake ya
kwanza toka ang'atuke katika chama cha CHADEMA.
Shilole bado ana nia ya kugombea ubunge kwenye jimbo lake la Igunga, lakini anahofia kuwa maisha yake yanaweza kuwa hatarini!
Shilole ameiambia Bongo5 kuwa amepokea simu nyingi kutoka Igunga
zinazomtaka ajitose kuwania nafasi hiyo, lakini bado yupo njia panda.
“Unajua siasa ni ngumu mimi bado nipo kwenye mjadala wa kugombea na
hii ni baada ya kuona watu wanataka kuongozwa, lakini bado nafikiria,”
amesema. “Nikiwa tayari nitagombea kupitia CCM. Kitu ambacho
kinaniogopesha kiukweli ukiangaliwa watu waliopita ni vijana tu wanakufa
mapema kutokana na mambo ya siasa. Siasa inahitaji moyo sana mimi ni
muoga sana, naogopa kufa watu wanauwana! Mtu unatamani lakini ndo hivyo,” ameongeza.
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limetangaza mgawo wa umeme kwa siku
tisa katika baadhi ya maeneo kutokana na upungufu wa nishati hiyo katika
Gridi ya Taifa.
Hali hiyo imetokana na maombi ya Kampuni ya Pan African Energy (PAT)
inayosimamia uzalishaji wa gesi asilia Songosongo kusimamisha uzalishaji
kwa nyakati tofauti ili kufanya matengenezo na kubadilisha baadhi ya
vifaa kwenye mitambo yake.
Taarifa ya shirika hilo kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana ilisema
shughuli hiyo itafanyika kwa siku tofauti kati ya Aprili 6 na Mei 10.