TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa, Uchaguzi Mkuu utafanyika
kama ulivyopangwa na haiwezi kusegeza mbele tarehe ya uchaguzi huo
kutokana na suala hilo kuwa ni la kikatiba.
 |
| Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji
Mstaafu Damian Lubuva akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar
es Salaam, kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Manunuzi na Logistic, Gregory
Kaijage na kushoto ni Naibu Katibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na
Mkuu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), Sisti Chriati. |
Akizungumza na
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Tume ya
Taifa ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema
kuwa wanasiasa wamekuwa na kauli ambazo zinawafanya wananchi wapate hofu
wakati suala hilo kuhairisha uchaguzi halipo katika tume.
 |
| Baadhi ya Wandishi wa habari waliohudhuria katika mkutano wa habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi jijini Dar es Salaam. |
jaji
Lubuva ameongeza kuwa wanasiasa wanatakiwa kuangalia maneno ambayo
wanayatoa kwani hayana msingi, wanatakiwa watoe sera zao za vyama kwa
wananchi na sio kuisemea tume mambo ambayo hayana ukweli wowote.