Showing posts with label UCHAGUZI MKUU HAUTASOGEZWA MBELE. Show all posts
Showing posts with label UCHAGUZI MKUU HAUTASOGEZWA MBELE. Show all posts

Sunday, 19 April 2015

NEC: UCHAGUZI MKUU HAUTASOGEZWA MBELE

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa, Uchaguzi Mkuu utafanyika kama ulivyopangwa na haiwezi kusegeza mbele tarehe ya uchaguzi huo kutokana na suala hilo kuwa ni la kikatiba.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Manunuzi na Logistic, Gregory Kaijage na kushoto ni Naibu Katibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Mkuu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), Sisti Chriati.

 Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema kuwa wanasiasa wamekuwa na kauli ambazo zinawafanya wananchi wapate hofu wakati suala hilo kuhairisha uchaguzi halipo katika tume.
Baadhi ya Wandishi wa habari waliohudhuria katika mkutano wa habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi jijini Dar es Salaam.
jaji Lubuva ameongeza kuwa wanasiasa wanatakiwa kuangalia maneno ambayo wanayatoa kwani hayana msingi, wanatakiwa watoe sera zao za vyama kwa wananchi na sio kuisemea tume mambo ambayo hayana ukweli wowote.