| Mwimbaji wa muziki wa Injili, Emmanuel Mbasha. |
“Yeah, ni kweli kaka, Flora ameamua kwenda mahakamani kudai talaka yake, sioni kama ni tatizo, kwa sasa siwezi kuzungumza lolote kwa sababu limeshafika katika mkondo wa sheria na tunapaswa kusubiri tuone kitakachotokea, lakini naamini kila kitu kitakwenda sawa,” alisema Mbasha.
Kwa upande wake, mke wa mwimbaji huyo, ambaye pia ni mkali wa nyimbo za gospo, Flora Mbasha alipotafutwa hakupokea simu yake ya mkononi, lakini alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno (sms) alijibu kwa kifupi:
“Kaka, naendesha, kila kitu kiko mahakamani kwa hiyo sina la kuzungumza kwa sasa.”
Hali hiyo inatokea siku chache tu baada ya mahakama hiyo kumuachia huru mwimbaji huyo aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka ya ubakaji ambayo pia yalimleta mkewe huyo mahakamani akiwa shahidi wa upande wa mashtaka.
Kwa muda mrefu, waimbaji hao wamekuwa katika mgogoro wa kifamilia ambapo juhudi za watu mbalimbali zimefanyika kusuluhisha lakini hazikufanikiwa.
No comments:
Post a Comment