MZEE mwenye umri wa miaka 68, Celestine Mushi, mkazi wa kata ya
Motamburu wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, ameuawa na wananchi
wanaotajwa kukasirishwa na kitendo chake cha kupeleka waganga wa jadi
kijijini kwa lengo la kuifanyia zindiko nyumba yake.

Mushi anadaiwa kuwatoa waganga hao wawili jijini Dar es Salaam na kuwapeleka Rombo kwa kazi hiyo maalumu.