Friday, 10 July 2015

All Afrika Games CAF yataja makundi

Upangaji wa makundi wa soka ya wanawake ya Michezo ya Afrika (All Africa Games) itakayofanyika nchini Congo Brazzaville kuanzia Septemba 4-19 umefanywa na Shirikisho la soka barani Afrika, CAF na timu ya taifa ya soka ya wanawake ya Tanzania, Twiga Stars imepangwa Kundi A pamoja na wenyeji Kongo, Nigeria na Ivory Coast.

 




Upangaji wa makundi hayo umefanyika leo makao makuu ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) mjini Cairo, Misri. Kundi B lina timu za Cameroon, Afrika Kusini, Ghana na Misri. Upande wa wanaume, Kundi A lina timu za Kongo, Sudan, Zimbabwe na Burkina Faso, wakati Kundi B kuna Ghana, Senegal, Misri na Nigeria.

No comments:

Post a Comment