Waziri mkuu wa Ugiriki, Alexis Tsipras amesema benki za nchi hiyo na masoko ya hisa yataendelea kufungwa na kudhibiti mitaji.
Katika
hotuba yake aliyoitoa kupitia televisheni, Bwana Tsipras ameomba kuwepo
na utulivu, hakusema kufungwa kwa shughuli za kibenki kutadumu hadi
lini, lakini amewahakikishia watu kuwa akiba zao, mishahara na malipo ya
pensheni ni salama.
Bwana Tsipras ameishutumu Benki Kuu ya Ulaya, ECB, kwa ulaghai juu ya uamuzi wake wa kutotoa fedha za dharura kwa Ugiriki.
Hatua
ya ECB inafuatia kuvunjika kwa mazungumzo ya Jumamosi kati ya Ugiriki
na nchi zinazotumia sarafu ya Euro juu ya makubaliano ya kuinusuru
Ugiriki kutokana na madeni yake yaliyopewa muda wa utekelezaji kufikia
Jumanne.
No comments:
Post a Comment