Manusura hao wamepokelewa katika kisiwa cha Sicily na maafisa wa usalama na wale wa uhamiaji waliowapiga picha na kuchukua majina yao.
Awali Shirika la Umoja wa mataifa, lilitoa wito kwa juhudi zaidi zifanywe ili kuokoa maisha ya wahamiaji wanaojaribu kufika bara Ulaya kutokea Kazkazini mwa Afrika.
Zaidi ya wahamiaji 400 wanahofiwa kufa maji baada ya boti walilokuwa wakilitumia kuzama siku ya Jumatatu katika bahari ya Mediterenia.
Msemaji wa umoja wa mataifa anayejishughulika na wakimbizi Laurens Jolles ameiambia BBC kuwa, juhudi za sasa za kujaribu kuwaokoa wahamiaji ni chache mno.
No comments:
Post a Comment