Saturday, 11 April 2015

Pellegrini:Mancity haipo katika mgogoro

Mkufunzi wa kilabu ya Manchester City Manuel Pellegrini amesisitiza kuwa kilabu yake haiko katika mgogoro .
Pellegrini
Raia huyo wa Chile anatapatapa kukoa kazi yake kama mkufunzi huku timu hiyo ikipambana na Manchester United siku ya jumapili katika mechi ya debi itakayochezwa uwanjani Old Trafford.
Manchester City imeshuka hadi nafasi ya nne kufuatia msururu mbaya wa matokeo baada ya kushinda mara mbili pekee kati ya mechi saba.

Kocha Pellegrini amewaona wapinzani wake Arsenal na Manchester United wakipanda katika jedwali katika majuma ya hivi karibuni na sasa anajua kwamba atasalia kuwa mkufunzi wa kilabu hiyo iwapo atafanikiwa kuiweka timu hiyo katika nne bora zitakazofuzu katika mashindano ya kuwania kilabu bingwa Ulaya msimu ujao.

No comments:

Post a Comment