viongozi wa vyama vitano vya upinzani wameshiriki katika mdahalo wa pili wa moja kwa moja ulioandaliwa na BBC.
Katika
hoja za kwanza, kiongozi wa chama cha Labour, Ed Miliband, amesema
suala la familia za wafanyakazi atalipa kipaumbele kwanza, wakati
kiongozi wa UK Independence Party,UKIP, Nigel Farage amesema atasaidia
biashara ndogo ndogo.Bwana Miliband, amesema anatarajia kupata ushindi mkubwa na hataunda serikali ya mseto na chama cha SNP.
Wagombea hao wamekuwa wakipingana katika masuala mbalimbali wakati wa mdahalo huo.
Waziri mkuu David Cameron wa chama tawala cha Conservatives na naibu waziri mkuu wake kutoka chama cha Lib Dem, Nick Clegg hawakushiriki katika mdahalo huo wa wazi.
No comments:
Post a Comment