Friday, 26 June 2015

Upinzani kususia uchaguzi mkuu Burundi

Nchini Burundi hali ya kisiasa inaendelea kutokota, huku vyama vya upinzani vikitangaza kususia uchaguzi mkuu unaotarajiwa kuanza wiki ijayo.
Ban Ki-Moon ametoa wito kwa utawala wa nchi hiyo kuhairisha uchaguzi mkuu
Makundi ya asasi za kiraia yamewaomba raia wa nchi hio kususia kura hio, huku Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon akitaka uchaguzi mkuu wa Burundi kuahirishwa.

Makundi ya kutetea haki za kibinadamu nchini Burundi yametoa wito kwa wapiga kura nchini humo kususia uchaguzi wa ubunge unaotarajiwa kufanyika siku ya Jumatatu.
Mashirika hayo yamesema kuwa kwa sasa mazingira ya kisiasa nchini humo hayawezi kuruhusu uchaguzi huru na wa haki, kufuatia miezi kadhaa ya ghasia.

No comments:

Post a Comment