Serikali ya Ugiriki imethibitisha
kuwa benki zake zitafungwa kwa kipindi cha juma moja kufuatia uamuzi wa
Benki kuu barani Ulaya wa kutoendelea kutoa fedha za kukabiliana na
dharura.
Utoaji wa fedha katika mashine za ATM utadhibitiwa huku watu wakiruhusiwa kutoa Yuro sitini kwa siku,hatahivyo masharti hayo hayatawaathiri raia walio na kadi za benki za kigeni.
Katika hotuba iliopeperushwa na runinga za taifa hilo Waziri mkuu nchini Ugiriki Alexis Tsipras ameomba utulivu.
No comments:
Post a Comment