Friday, 10 April 2015

BAADA YA TAMKO LA WAZIRI DALADALA JIJINI DAR ZAANZA KAZI

TAMKO la Waziri wa Kazi na Ajira, Mhe. Gaudencia Kabaka la kufuta agizo lililokuwa likiwataka madereva wa mabasi na malori kwenda kusoma katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) limesababisha madereva waliogoma kusafirisha abiria kwenye daladala kuanza kazi za kusafirisha abiria leo mchana.

Waziri Kabaka alisema mchana huu kwamba serikali pamoja na madereva wamekubaliana kukutana Aprili 18 mwaka huu kwa ajili ya kuzungumza njia mbadala ambayo inaweza kuwasaidia katika kutatua tatizo hilo. Waziri alilitaka jeshi la polisi nao kuondoa tochi za barabarani ambazo zilikuwa moja ya kero ya madereva barabarani.

No comments:

Post a Comment